• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Newala Mji yatumia zaidi ya shilingi bilioni 2 kutekeleza miradi ya maendeleo

Posted on: May 8th, 2019

Halmashauri ya mji Newala mkoani Mtwara hadi kufikia Machi 31, 2019, imetumia shilingi bilioni 2.28 kutekeleza miradi ya maendeleo fedha ambazo ni sehemu ya shilingi bilioni 2.29 ilizopokea kutekeleza miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 4.81 kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Hayo yameelezwa kwenye kikao cha baraza la Madiwani la halamashauri hiyo cha robo ya ya tatu kilichofanyika Machi 3 na 6 2019, katika ukumbu wake wa mikutuno mjini Newala ambapo imeelezwa kuwa shilingi bilioni 1.47 ni fedha zilizopokelewa mwaka wa fedha 2018/2019 na shilingi milioni 807 ni fedha za bakaa ya mwaka wa fedha 2017/2018.

Aidha makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho  Mhe. Othuman Bilali amewaomba madiwani kushirikiana na watendaji wa serikali kusimamia, kuhimiza na kuwaelimisha wananchi juu ya ulipaji wa tozo mbalimbali za kisheria kwani hali ya mapato ya ndani ni mbaya hivyo nguvu ya pamoja ya ukusanyaji mapato inahitajika ili halmashauri iweze kujiendesha.

Aidha katika hatua nyingine amesema hamlamashauri imepokea kwa mikono miwili taarifa ya kupata hati safi na kuahidi kuendelea kuwasimamaia wataalam katika kutekeleza shughuli za miradi ya maendeleo kwa kufuata taratibu zinazokubalika na kwa uadilifu ili kuitetea hati hiyo kwa mara nyingine.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halamashauri Ndg. Andrew Mgaya amefafanua kuwa hali ya mapato ya ndani hairidhishi hivyo amewaomba madiwani kusaidia kutoa uelewa kwa wananchi wao kusuhu vyanzo vipya vya mapato vilivyoanishwa hasa anuwani za makazi na vibali vya ujenzi ambapo kwa sasa kila mwananchi enayefanya ujenzi kwenye eneo lake ni lazima awe amelipia kibali.

Mgaya amefafanua kuwa vibali hivyo vya ujenzi vinatolewa kwa mtu yoyote anayeendeleza ardhi yake kwa kufanya ujenzi katika eneo lote la halmashauri ya mji, na kwa kufanya hivyo itasaidia kuepusha matatizo yanayoweza kujitokeza kutokana na ujenzi holela pamoja na kusimamia sheria za mipango miji.

Akizungumza katika mkutano huo Mkuu wa wilaya Newala Mhe. Aziza Mangosongo amewata madiwani kutambua ajenda ya mapato ndio ajenda kuu katika halmashauri kwani bila mapato hakuna halmashauri na hata takwimu za sasa za kitaifa zimeonyesha halmashauri  ipo nafasi ya 157 kati ya halamshauri 185 hivyo jitihadi zaidi zinaitajika kuongeza ukusanyaji.

Mhe. Mangosongo pia amesema suala la vitambulisho vya wajasiriamali wadogo ni la kitaifa hivyo kila mmoja aone umuhimu wa kuwahimiza walengwa kujitokeza kuchukua vitambulisho hivyo kwani baada ya kumaliza kuuza vitambulisho elfu 5 vya awamu ya kwanza, awamu ya pili wilaya imepewa vitambulisho elfu 13 na vilivyouzwa hadi sasa havijafika elfu 5.

Sambamba na hilo Mkuu wa wilaya ameipongeza halmashauri kwa kupata hati safi na kushika nafasi ya kwanza kimkoa nafasi ya 4 kikanda na ya 6 kitaifa  katika mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2018, na kuitaka halmashauri kuendeleza utendaji bora wa kazi ili kuzitetea nafasi hizo.




Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa