• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

TASAF imetoa shilingi milioni 101 kujenga zahanati kijiji cha Msilili

Posted on: July 18th, 2023

Wakazi wa Kijiji cha Msilili Kata ya Mcholi II Halmashauri ya Mji Newala mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kupitia mradi wa Mpango wa kunusuru Kaya Maskini Nchini (TASAF) kwa kutekelezea mradi wa zahanati katika kijiji chao umbao utawanufaisha watu 6,000.

Wakazi hao wametoa shukrani hizo Jumanne 18/07/2023 kijiji hapo wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Kazi Maalum na Mbunge wa jimbo la Newala Mjini Mhe. George Mkuchika ya kuongea na wananchi kuhusu maendeleo yanayofanywa  na serikali pamoja na jimbo.

Mwenyekiti wa kijiji hicho Ndg. Abdulazizi Chapacha amemwambia Mhe. Waziri kuwa wanaishukuru serikali kupitia TASAF kwa kuliona hitaji lao la mda mrefu na kutoa fedha shilingi milioni 101 kutekeleza mradi huo ambao ni mkombozi kwa wananchi wa Msilili kwa huduma za afya.

Mwenyekiti huyo amesema wananchi kwa nguvu zao waliwahi kujaribu kujenga zahanati kwa nguvu zao lakini wahakuweza, “tuliwahi kujaribu kujenga kwa nguvu zetu lakini hatukufika pote, kwakwli tunaishukuru serika tunamshukuru Rais wetu Samia pamoja na TASAF, sisi wananchi tupo pamoja na Serikali ya Mama Samia”. Alieleza Ndg. Chapacha.

Kwa uapande Waziri Mkuchika amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo anawatumikia watanzania na wananchi huku akiwaomba wananewala kuendelea kumuunga mkono mheshimiwa Rais ili wazidi kuona matunda ya awamu ya utumishi wake.

Bi. Sophia Mkatenda mkazi wa kijini hapo amesema TASAF imekua kama mkombozi kijiji kwao kwa kuwa walikua wanatembea kilometa 8 kufuata huduma za afya hali ambayo alikua ni Changamoto hasa kwa wanawake wajawazito.

Bw. Mustafa Chilumba mjumbe wa serikali ya kijiji ametoa pongezi kwa mbunge wao kwa uwakilishi wake wa kutoa msukumo wa kupata miradi ya maendeleo katika jimbo lake. “kwanza tunaishukuru serikali na haya yote yanafanyika kutokana na kuwa na mbunge anaetusemea vizuri, tunamshukuru mbunge wetu”. Alisema kiongozi huyo.

Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji Newala Ndg. Alphayo Zakaria amesema mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Msilili umetokana na uhitaji wa wananchi wenyewe ambao waliibua wakati wa mapendekezo na TASAF iliona ni mradi sahihi sambamba na mradi wa kisima unaotarajiwa kutekelezwa kwa wastani wa shilingi milioni mbili.

Zakaria amepongeza mwitikio wa wanamsilili ambao amesema wametoa ushirikiano wa asilimia 100 katika utekelezaji wamejitoa kikamilifu na kuleta maana halisi ya ushiriki wa jamii katika shughuli za maendeleo huku akibainisha kuwa ujenzi wa zahanati hiyo upo kwenye hatua ya umaliziaji.

“Wananchi mradi huu wameutekeleza kwa kujitosheleza, wamejitoa kwa asilimia zote, kile ambacho wametakiwa wajitolee wameonyesha mchango ambao ni nguvu za jamii kwa kiwango kinachotakiwa kinachorisha nakupitiliza hari walio ionesha wasiiache.” Alieleza Zakaria

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa