• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Viongozi wa dini wametakiwa kuwa chachu ya mabadiliko ya kukomesha ukatili katika jamii

Posted on: August 30th, 2022

Viongozi wa dini wa Halmashauri ya Mji Newala wametakiwa kuwa chachu ya mabadiliko ya kukomesha ukatili katika jamii na kusaidia malezi bora ya watoto ambao sasa wapo hatarini kutokana na kukithiri kwa matendo ya unyanyasaji.

Wito huo umetolewa  na Mkuu wa Wilaya Newala  Alhaj Rajabu Kundya wakati anafungua warsha ya ulinzi wa mtoto kwa viongozi wa dini, kamati ya ulinzi na usalama, wakuu wa shule na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa mtoto ya halmashauri ya Mji Newala.

Alhaj Kundya amesema kwa sasa kuna ongezeko kubwa la vitendo vya ukatili ambavyo vinatishia ukuaji wa watoto, hivyo malezi ya kiroho ndio njia muhimu itakayosaidia kubadilisha hali hiyo na kumfanya mtoto kuwa salama kimwili na kiakili.

Jamii yetu inavyobadilika inakwenda kwenye mabadiliko hasi maana yake tuanalegalega katikakutekeleza wajibu wetu na hivyo kuumba jamii ya watu ambao wamekata tama, watu wanaoishi kama wanyama na wasio namanufaa kwao wenyewe, kwa jamii yao na kwa taifa lao. Alisisitiza Kundya

Akiongea katika warsha hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Newala Bi. Shamim Mwariko amesema viongozi wa dini ndio msingi wa ustawi wa jamii katika kuleta amani kuanzia ngazi ya familia mpaka Taifa kwa kuwa na viongozi na wananchi waadilifu.

Bi. Mwariko amefafanua kuwa kiongozi wa dini ana mamlaka ya kimungu inayosikilizwa na watu hivyo ni chombo muhimu kinachotegemewa katika kuimarisha mahusiano mema katika jamii kwa kuwawekea ulinzi watoto ili kujenga maadili yasiyoharibika na kuliendeleza taifa.

Akiongea kwa niaba ya vyombo vya ulinzi na usalama Mwakilishi wa Kamanda wa Polisi wilayani Newala OC-CID ASP Idd Omary amewataka viongozi wa dini kujiepusha na imani za itikali kali ambazo mara nyingi zinakuwa si za kizalendo na kubeba malengo ya uvunjifu wa amani.

Aidha ASP Omary ameeleza kuwa dini ndilo eneo hatarishi kwa amani ya Tanzania endapo viongozi wake hawatasimama imara katika kujenga umoja na mshikamano hivyo ni muhimu kuwa waangalifu katika kutumia majukwaa mbalimbali pamoja na kuhakiki mafundisho yanayotolewa kwa watoto kwenye makanisa na misikiti.

Mwenyekiti wa kamati ya amani na maridhiano ya wilaya ya Newala ambaye pia ni Shekhe Mkuu wa wilaya Yusufu Mikidadi amekiri kuwa jamii imeyumba kwenye ulinzi na malezi ya watoto kutokana na utandawazi pamoja na muda mwingi kutumika shuleni ambako hawapati malezi ya kiroho.

Mchungaji Atupakisye Ngonyani wa kanisa la EFATHA amesema pamoja na viongozi wa dini kubeba mzigo huo lakini serikali kupitia vyombo vyake nayo isimame katika nafasi yake ya kutofumbia macho matendo maovu ili jamii iwe salama kimwili na kiroho.

Warsha ya siku moja iliandaliwa na kitengo cha Ustawi wa Jamii halmashauri ya Mji Newala ililenga kujadili mada tatu ambazo ni Usalama ni jukumu la viongozi wa dini katika kuendeleza na kuimarisha amani, Ulinzi na usalama wa mtoto pamoja na Mabadiliko ya tabia Nchi.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI MAKARANI WA SENSA, MSIMAMIZI WA MAUDHUI NA MSIMAMIZI WA TEHAMA July 19, 2022
  • TANGAZO MIKOPO YA VIWANJA NA MATOFALI October 12, 2021
  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya fedha yataka wananchi kujilinda njaa kutokana na uhaba wa mvua na mafuriko

    March 23, 2023
  • Wakuu wa Idar na Vitengo wametakiwa kuacha upendeleo kwa watumishi wasiowajibika kazini

    March 20, 2023
  • Jamii, Wadau, Mashirika na wasimamizi wa sheria wametakiwa kijikita katika kuzuia ndoa za utotoni

    March 11, 2023
  • Halmashauri ya Mji Newala yashauriwa kuwekeza katika elimu ya matumizi ya mfumo wa TAUSI

    March 08, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa