• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Viongozi wa kata na vijiji wanatakiwa kusimamia upatikanaji wa chakula shuleni

Posted on: May 9th, 2023

Viongozi wa kata na vijiji Halmshauri ya Mji Newala wametakiwa kusimamia ukusanyaji na upatikanaji wa chakula shuleni pamoja na kuhakikisha usalama  wa chakula wanachopatiwa wanafunzi.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya Newala Mhe. Mwangi Rajabu Kundya Mei 08, 2023 wakati akizungumza na wajumbe wa kamati ya kikao cha kujadili utekelezaji wa afua za lishe ngazi ya Kata kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Mhe. Kundya ameeleza kuwa upatikanaji wa chakula kwa watoto shuleni kutaongeza umakini wa mtoto wakati wa kujifunza na kuimarisha afya ya akili hivyo viongozi wahamasishe wazazi kutambua umuhimu huo na kuchangia chakula bila shuruti

Aidha Mhe. Kundya ameelekeza waandaaji wa chakula lazima wazingatie usalama na afya za watumiaji kwa kuhifadhi na kuandaa chakula katika mazingira salama “laikini kingine ni hayo mazingira, mazingira ya usafi maana shuleni ndipo kilipo kitovu cha elimu, elimu ni pamoja na utaratibu wa chakula kwa nia ya kulinda afya zao”. Alieleza Mhe Kundya.

Katika kuhakikisha shule zinatoa huduma ya chakula kwa wanafunzi wawapo shuleni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Yusuph Kateule amewaagiza maafisa watendaji wa kata kwenda kuzisimamia shule zote zenye maeneo ya wazi zianze kuzalisha chakula kwa kulima mazao mbalimbali ya chakula. 

Aidha ameongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kuanza kujenga mtazamo kwa wazazi kuona umuhimu wa kuchangia chakula na itapunguza kiasi cha wingi wa uchangiaji kwa kuwa shule zenyewe zitakua zimeonyesha njia.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Shamimu Mwariko amesisitiza utaratibu wa utunzaji wa chakula uzingatiwe kwa kuhakikisha kinakaushwa na kuhifadhiwa sehemu salama itakayowezesha kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika.

Hata hivyo amemtaka afisa lishe kuweka mpango wa kutembelea shule kujiridhisha juu ya hali ya ulaji wa watoto kwani wanaweza wakawa wanakula chakula kisicho na msaada wa kiafya na kimwili kutokana na mazingira mabovu ya utunzaji na uhifadhi, “Vyakula vinapoletwa shuleni vikaushwe katika kiwango kinachotakiwa viweke katika mifuko ya design ya kinganjaa au ya A to Z kwasababu ina uwezo wa kuweka hata miaka mitatu.” Alisisitiza

Kikao hicho cha robo ya 3 2022/2023 kiliketi kutathmini utekelezaji wa mkataba wa afua za lishe ngazi ya Kata kwa kata zote 16 za Halmashauri ya Mji Newala na katika kupitia taarifa zake ilionyesha baadhi ya shule hazitoi chakula na kuweka azimio la kuchangisha vyakula kwa wazazi.



Matangazo

  • TANGAZO MIKOPO YA VIWANJA NA MATOFALI October 12, 2021
  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji ataka ulinzi wa watoto kwa kufunika visima vya maji

    May 11, 2023
  • Idara ya Afya yatakiwa kusimamia mpango wa Taifa wa udhibiti malaria

    May 10, 2023
  • Viongozi wa kata na vijiji wanatakiwa kusimamia upatikanaji wa chakula shuleni

    May 09, 2023
  • Wananchi wa Tarafa ya Mkunya waishukuru Serikali kwa kuwaboreshea huduma za afya

    May 04, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa