• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

WALIMU KIDATO CHA SITA WAPONGEZWA KWA MATOKEO MAZURI

Posted on: July 30th, 2025

Wakuu wa shule na walimu wa kidato cha sita Halmashauri ya Mji Newala wamepongezwa kwa jitihada zao za kuhakikisha wanafunzi wanafanya vizuri katika mtihani wao wa taifa mwaka 2025.

“Kwanza niwapongeze walimu wetu pamoja na wakuu wa shule kwa jitihada za dhati kabisa walizochukua katika kipindi hiki mpaka kupata matokeo haya, baadhi ya shule zilikuwa ndo zinaanza, baadhi ya walimu hawakuwa waozefu”. 

Pongezi hizo zimetolewa na kaimu mkuu wa idara ya elimu sekondari Mwl. Innocent Kerenge kufuatia matokeo ya jumla waliyoyapata katika shule  zake nne, mbili za wasichana zenye mchepuo wa sanaa na mbili za wavulana za mchepuo wa sayansi.   

Kerenge amefafanua “Kati ya wanafunzi 408 waliofanya mtihani, waliopata daraja la kwanza ni 107 sawa 26%, waliopata Daraja la pili ni wanafunzi 262 sawa 64% ni wanafunzi 39 pekee waliopata daraja la tatu sawa  na 10% hakuna daraja la nne wala sifuri katika shule zetu”.

Aidha Mwl. Kerenge amesema ni mpango wa halmashauri kuongeza ufaulu na kuondoa daraja la tatu, la nne na daraja sifuri huku akiishukuru serikali kwa kuwaongezea walimu wapya wataalam wa maabara, vifaa vya maabara pamoja na vitabu.

Kwa upande wake mwalimu wa somo la Historia katika shule ya sekondari ya wasichana Nangwanda Mwl. Happyness Haule amefurahishwa na matokeo hayo na kuwataka wanafunzi wanaotarajia kufanya mtihani ujao kuwa tayari kwa ajili ya mpango wa ufaulu wa juu zaidi.

Naye mwalimu wa fizikia na kemia katika shule sekondari ya wavulana Nambunga Mwl. Jonas Mgonya amekiri changamoto ya ugeni katika kufundisha kidato cha tano na sita kwani walimu wote shuleni hapo walikuwa wapya.

Hata hivyo Mwl. Mgonya amefurahishwa na serikali kumleta mtaalam maabara shuleni hapo “matokeo yaliyopita hatukua na mtaalamu wa maabara hivyo utatusaidia kuwainua hawa vijana kwa kufanya majaribio mengi ya vitendo yakutosha hivyo kuwezesha matokeo mazuri”.

Halmashauri ya Mji Newala ina shule nne za sekondari za kidato cha tano na sita shule sekondari ya wasichana Nangwanda, shule sekondari ya wasichana Kiuta, shule mbili mpya za wavulana zilizofanya mtihani kwa mara kwanza shule ya sekondari Nambunga pamoja na Malocho.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Fedha za mfuko wa elimu shilingi milioni 155 zatekeleza miradi ya elimu Newala Mji

    July 31, 2025
  • WALIMU KIDATO CHA SITA WAPONGEZWA KWA MATOKEO MAZURI

    July 30, 2025
  • Mkurugenzi Nnauye amewapongeza wataam wa afya na watendaji wa kata utekelezaji mkataba wa lishe

    July 30, 2025
  • WANAUME WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI MASUALA YA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    July 02, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa