• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wananchi wa Halmshauri ya Mji Newala wametakiwa kuchukua tahadhari za kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya mlipuko

Posted on: March 31st, 2023

Wananchi wa Halmshauri ya Mji Newala wametakiwa kuchukua tahadhari za kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya mlipuko kufuatia kuenea kwa ugonjwa wa kichocho katika vijiji vya kata ya Mcholi I, Mcholi II na Mtumachi.

Rai hiyo imetolewa Machi 30, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Mwangi Rajabu Kundya kwenye kikao maalum cha kamati ya Afya ya Msingi kilichoketi kujadili mlipuko huo uliojitokeza hivi karibuni.

Mhe. Kundya amewataka wananchi kuchukua tahadhari ya ugonjwa huo wakati taratibu za utoaji wa chanjo zikiendelea kwa kuwa madhara yake ni makubwa kiafya na uchumi.

“Ugonjwa huu ni hatari na unaathiri sio tu kwa afya pekeyake hata uchumi wa eneo husika unaathiriwa, hivyo tunawaomba wananchi wachukue tahadhari za kujikinga na maambukizi wakati taratibu za utoaji wa chanjo kwa wananchi wote zikifuatiliwa”Alifafanua Kundya

Hata hivyo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Yusuph Kateule amewaomba viongozi wa vijiji, kushirikiana na viongozi wa dini katika maeneo yao kuongea na wananchi juu ya madhara ya ugonjwa wa kichocho na kuwashirikisha wataalamu wa afya katika utoaji elimu hasa juu ya umuhimu chanjo zinazotolewa.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Hospital ya Halmashauri ya Newala Dkt. Ramadhani Shabani amewasisitiza wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya mlipuko huo huku akieleza madhara yake kuwa ni makubwa ikiwemo kuvimba tumbo, figo kuharibika, saratani ya kibofu, matatizo ya moyo, kushindwa kufanya kazi pamoja na kifo.

Aidha imeelezwa kuwa rahisi kupata maradhi hasa katika kipindi hiki cha mvua kwa kuwa vimelea uenea kwa njia ya mkojo au maji yaliyochanyika na mkojo wa muathirika hivyo ni wakati wa kutunza mazingira yawe safi, kwa kukata nyasi na kufukia vidimbwi vya maji vinavyoweza kusababisha kuzaliana kwa vimelea vya kichocho.

Akiongea wakati anafunga kikao hicho Mkuu wa Wilaya amewataka  viongozi wa kata na vijiji na wananchi kwa ujumla kujianda kupokea chanjo za ugonjwa huo  siku chache tu baada ya kumaliza mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa