• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

WANAUME WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI MASUALA YA AFYA NA LISHE YA MTOTO

Posted on: July 2nd, 2025

Katika kuadhimisha awamu ya pili ya mwezi wa siku ya afya na lishe ya mtoto Juni 2025, halmashauri ya Mji Newala, wanaume wametakiwa kukijitokeza kushiriki katika masuala ya afya na lishe ili jamii iwe na malezi mazuri sambamba na kuimarisha matokeo bora ya ukuaji wa watoto.

Hayo yameelezwa na Bw. Mwistala Lazima kutoka kijiji cha Kazamoyo kata ya Mnekachi katika halamshauri hiyo ambaye ameeleza kuwa wanaume kujitokeza katika siku za maadhimisho ya lishe ni njia mojawapo ya kuimarisha malezi ya familia.

“Mimi kama mzazi inanilazimu niwe na upendo kwa familia yangu hivyo niwasisitize wanaume wenzangu wawe wanashiriki kwenye haya mazoezi yaani wasiwe wazembe hii inaweza ikasaidia pia kuwa walezi bora kwenye familia zao”.

Aidha Bw. Lazima amefafanua kuwa anatambua ukuaji nzuri wa mtoto unatokana na upatikanaji wa lishe bora na hiyo ndio sababu ya yeye kujitokeza mara zote yanapofanyika maadhimisho hayo kwa lengo la kupata elimu itayoisaidia familia yake.

Naye Bi. Ashura Mnipela mmoja wa wanawake waliodhuria siku hiyo amewaomba wamama kuwa mstari wa mbele katika kuhamasika na kuzingatia masuala ya afya na lishe ya mtoto kwa kuwa inasaidia kuimarisha ukuaji.

“Mimi nimeona watoto walikua awaongezeki kwa kilo sasa angalau ninapojifunza mambo ya lishe na jinsi ya kupika angalau wanaongezeka uzito pia, lakini pia nawahamasisha na wanawake wenzangu wengine hapa hawapo wapo mashambani wasiwe na moyo huo, tuendelee kuambatana na hamasa hizi za lishe”.

Kwa upande wake Afisa lishe wa halmashauri ya Mji Newala Bi. Beatrice Saria amebainisha kuwa maadhimisho ya mwezi wa siku ya afya na lishe ya mtoto yanawahusisha watoto wa chini ya miaka mitano na yanafanyika mara mbili kwa mwaka, mwezi wa sita na mwezi wa kumi nambili.

 Hata hivyo Bi. Saria ameeleza kuwa katika awamu hii wamezifikia kata zote 16 kutoa matone ya vitamini A, kutoa dawa za minyoo ya tumbo, kufanya tathmini ya hali ya lishe, mapishi darasa pamoja na kutoa elimu ya ulaji sahihi kwa kuzingatia makundi sita ya chakula.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANAUME WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI MASUALA YA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    July 02, 2025
  • HOSPITALI YA WILAYA YA NEWALA IMEANZA KUTOA MATIBABU YA VIUNGO KWA NJIA YA MAZOEZI

    July 01, 2025
  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa