• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wasimamizi wa huduma za mama na mtoto watakiwa kuhakikisha uzazi salama

Posted on: July 26th, 2023

Wataalam wa afya wanaosimamia huduma za mama mjamzito na watoto wachanga mkoani Mtwara wametakiwa kutambua lengo la Serikali la kuongeza vituo vya afya na majengo ya wazazi ni uhakika wa kuwa na uzazi salama.

Hayo yameelezwa Jumatano Julai 26, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Newala Alhaj. Mwangi Rajabu Kundya wakati anafungua kikao cha uchunguzi wa vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga mkoani Mtwara kilichofanyika kwenye ukumbi wa Chuo Cha Uuguzi Newala.

Alhaj. Kundya amesema serikali imeongeza vituo hivyo ikilenga kuokoa maisha ya mtoto mchanga pamoja na usalama wa wajawazito kwa kupata msaada wa kitaalam hasa pale inapojitokeza changamoto wakati wakujifungua.

Aidha amewataka wataalam hao kuonyesha thamani ya uwekezaji huo wa serikali kwa kuzingatia weledi wa kuwahudumia wananchi. “uwezekezaji huu utaleta tija endapo tuu.. watalam mtaboresha huduma za kitaalam kwa kuhakikisha mnatoa huduma kwa weledi, staha, kuwa na huruma na kuepusha lugha za kukatisha tama”. Alieleza Kundya.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara (RMO) Dkt. Hamad Nyembea, amesema mkoa umeamua kuandaa jukwaa hilo muhimu kufanya tathmini, kujipima pamoja na kuweka maazimio ya maboresho, kwa kuwa huduma za mama na mtoto mchanga ni kiashiria cha toaji huduma bora za afya kwa wananchi.

Dkt. Nyembea amesema kwa kuwa serikali imewajibika kwa vitendo kuboresha miundombinu kwenye sekta afya hivyo ni wajibu wao kupanga mikakati ya kupunguza hatari ya vifo na kutoa huduma bora hasa kwa wanawake wajawazito na watoto.

Hata hivyo ametaja malengo ya kikao hicho kuwa ni kupitia utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa kwenye kikao kilichopita, utendaji kazi katika huduma za akina mama na watoto pamoja na kuangalia idadi ya vifo na sababu zakutokea vifo hivyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Newala Ndg. Geofrey Mnauye amewataka washiriki wa kikao hicho kukitendea haki kwa kuchangia mawazo sahihi yatakayowezesha kuleta matokeo yaliyokusudiwa ya kuisaidia jamii na taifa kwa ujumla.

Aidha ameongeza kuwa majadiliano yalenge kumaliza tatizo lililopo na kupunguza mijadala ya mara kwa mara ambayo haina matokeo. “Matarajio yangu katika rotation hii tunazokwenda mwisho wa siku RMO tutakuwa na ziro report maana yake vikao vitapungua kwa kuwa tatizo litakuwa limepungua”. Alifafanua Mkurugenzi huyo.

Kikao hicho cha uchunguzi wa vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga mkoani Mtwara ni cha siku tatu kuanzia Julai 26-28, 2023 kikiwahusisha wataalam wa halmashauri zote 9 za mkoa, na kinafanyika kila baada ya miezi mitatu kwa mzunguko wa kila halmashauri kuandaa kikao hicho.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa