• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Watakiwa kutumia maarifa mbalimbali na mbinu bunifu za kuboresha hali ya lishe

Posted on: July 20th, 2023

Wadau wa lishe kwa kushirikiana na Maafisa watendaji wa Kata Halmashauri ya Mji Newala wametakiwa kutumia maarifa mbalimbali na mbinu bunifu za kuboresha hali ya lishe kwa jamii zitakazo fanikisha kufikia malengo ya serikali.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Mwangi Rajabu Kundya katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa afua za lishe ngazi ya kata robo ya nne 2022/2023 kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo siku ya Jumatano Julai 19, 2023.

Amesema watendaji wa kata kwa kushirikiana na wadau wanatakiwa kuweka mipango madhubuti ya kuhakikisha afua za lishe zinafikiwa kwa asilimia 100 ikiwa pamoja na kuazimisha siku yalishe, watoto wanapata chakula shuleni, kuzingatia makundi ya vyakula na mambo mengine yanayohusu lishe.

Mhe. Kundya amesema serikali inaendelea kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma za afya kwa kujenga hospitali ambazo pia zinazotoa huduma ya Mama na Mtoto zinazopelekea kuwa na Taifa la watu imara wenye utimamu wa akili.

“Mama samia anafanya jitihada kubwa sana ya kuhakikisha anatujengea hospitali zinazotoa huduma za mama na mtoto naomba nendeni mkatafakari na kutumia akili ya ziada kwenye kufanikisha malengo yetu.” Alisisitiza Mkuu wa Wilaya

Kwa upande wake Mratibu wa lishe wa Halmashauri ya Mji Newala Ndg. Enos Kuzenza ameiomba jamii kushirikiana na viongozi ngazi ya kata na vijiji kuhakikisha wanachangia chakula shuleni ili watoto waweze kuwa na uwezo wa kupokea maarifa wanayofundishwa.

Kuzenza amesema jamii itakikwa ibadilike kwani bado takwimu zinaonesha wanafunzi wengi wahapati chakula shuleni “Kupitia kikao hiki tumeona takwimu zinazoonesha kwamba asilimia ndogo ya wanafunzi wanakula shuleni na tumeona shule zinazotoa chakula niwasihi wazazi na jamii kuwezesha chakula shuleni”. Amefafanua Kuzenza.

Katika kikao hicho Mkuu wa wilaya alitoa zawadi ya cheti cha ubora kwa kata iliyofanya vizuri katika kutekeleza afua kwa robo ya nne Kata ya Mkote ndio iliyoibuka mshindi ambapo diwani wa kata hiyo Mhe. Hamisi Kazibure alipokea hati hiyo.

Mhe. Kazibure amesema zawadi hiyo chachu ya kuendelea kufanya vizuri na wamejipanga kwenda kuongeza kutoa elimu ya unyonyeshaji na ulaji majumbani na shuleni kwani jamii inayo vyakula vyote changamoto waliyonayo hawana elimu ya mpangilio wa vyakula hivyo.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA NEWALA IMEANZA KUTOA MATIBABU YA VIUNGO KWA NJIA YA MAZOEZI

    July 01, 2025
  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa