• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Watumishi wa serikali watakiwa kuwajibika kimalifu ili kufikia malengo ya serikali

Posted on: March 11th, 2019

Watumishi wa serikali nchini wametakiwa kuwajibika ipasavyo katika nafasi zao, ili kurahisha kufikia malengo tarajiwa na kutengeneza uhusiano nzuri baina ya wananchi na serikali.

Wito huo umetolewa mwishoni mwa juma lililopita 09th March 2019, mjini Newala na Naibu Waziri Ofisi ya Rais –Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (OR-TAMISEMI) anaye shughulikia Elimu,  Mhe. Mwita Waitara wakati anazungumza na watumishi wa serikali wa wilaya ya Newala kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Newala.

Mhe. Waitara alisema kila mmoja anapaswa kutambua nafasi aliyonayo ndio dhamana yake ya kiutumishi hivyo ni vema kuwajibika kwa kuzingatia taratibu, kanuni pamoja na matakwa ya kiutendaji ya ajira na mwajiri “hasa kwenye suala la muda, hakikisheni munatumia muda wa kazi wa serikali vizuri kwa kuwahudumia wananchi” alisisitiza.

Aidha Waitara alieleza watumishi watekeleze wajibu wao kwa kuangalia mahitaji ya wananchi na sio kufanyakazi kwa kuwaangalia viongozi hasa wanapokuwa kwenye ziara mbalimbali jambo ambalo halitavumiliwa “utakuta mtumishi haoni umuhimu wa kutatua kero fulani ya wananchi, mpaka asikie kuna kiongozi wa juu yake anakuja, wewe hautufai, tekeleza wajibu wako mambo mengine yaweke pembeni, kama unaitikadi nyingine za kisiasa hapa sio mahala pake, kwa kuwa upo kazini tekeleza kazi za serikali hakuna ugonvi”, aliongeza.

Hata hivyo aliyataja mambo matatu yanayoweza kusaidia utendaji bora kwa watumishi kuwa ni mahusiano mazuri kazini, uzalendo na mtumishi kujiamini katika nafasi yake na kuondokana na hofu kwani kufanya kazi bila kujiamini ni chanzo cha kuharibu utendaji wa kazi.

Akiongea awali wakati anamkaribisha Naibu Waziri huyo, Katibu tawala wa wilaya ya Newala (DAS) Bwana Daniel Zenda kwa niaba ya Mkuu wa wilaya, aliwataka watumishi wa serikali wilayani hapa kufanyakazi kwa bidii na kuzingatia uadilifu kazini.

Naibu Waziri huyo, yupo mkoani Mtwara tangu 06th March 2019 kwenye ziara yake ya kikazi ya kuzitembelea halmashauri zote tisa (9) za mkoa huu, kukagua miradi ya elimu na kuongea na watumishi wa serikali.


Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa