• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Waziri Mkuchika awataka Wadau wa elimu kushikamana katika kuhamasisha elimu

Posted on: April 1st, 2023

Mbunge wa Jimbo la Newala Mhe. George Huruma Mkuchika ambae pia ni Waziri Ofisi ya Rais Kazi Maalum amewataka madiwani na wadau wengine wa elimu kuhamasisha elimu katika maeneo yao kwani wao ndio daraja kuu la kuunganisha kati ya jamii na walimu.

Ameyasema hayo Machi 31, 2023 wakati akiongea na wadau wa elimu na wazazi waliohudhuria kwenye hafla ya kilele cha wiki ya elimu iliyofanyika kwenye ukumbi wa halmshauri ya mji Newala ambapo amewasisitiza wadau wa elimu kuzingatia lishe kwa kuhakikisha chakula kinapatikana shuleni ili kuwawezesha wanafunzi kusoma kwa utulivu.

Mhe. Mkuchika amesema ni lazima kuwa na nguvu ya pamoja kwa Viongozi na wazazi waungane kuhakikisha chakula cha kutosha kinapatikana shuleni na kwa kufanya hivyo mahudhurio ya wanafunzi yatakuwa mazuri hali ambayo moja kwa moja ujifunzaji utaongezeka na utoro utapungua.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Mwangi Rajabu Kundya amewapongeza walimu kwa jitihada wanazozifanya katika ufundishaji shuleni pamoja na jukumu kubwa la malezi walionalo watoto wawapo shuleni  na kuwasisitiza kuendelea kufanya hivyo kwa kuwa hiyo ndio taaluma yao.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Shamim Mwariko amewataka wadau wa elimu kwa kushirikiana na wazazi kuimarisha malezi ya watoto kimaadili ambayo kwasasa yanaonekana kushuka kutokana ulimwengu unavyokwenda jambo linalosababisha na masuala ya elimu kuporomoka hivyo umakini mkubwa unahitajika.

"Kila mmoja kwa nafasi yake anatakiwa kuwajibika katika kuwalinda watoto kutokana na kuporomoka kwa maadili katika jamii yetu. Kwa maana hiyo popote alipo mtoto, mzazi au mdau wa elimu bila kujali mtoto ni wako au sio wako lazima kumwangalia kwa jicho la tatu kwani chachu ya elimu inatokana na sisi walezi kuonesha nia ya watoto wetu kupata elimu"  Amesema mkurugenzi huyo

Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri Mwl. Athman salum, amesema serikali kwa upande wake imeshaweka mazingira rafiki ya miundo mbinu na licha ya upungufu wa walimu wanafunzi wamekua wakifanya vizuri hivyo walimu wanastahili pongezi kwa jitihata zao kwa kutoa elimu kutokana na  nguvukazi iliyopo.

Kwa upande wao baadhi ya wadau waliohuduria hafla hiyo Mwl. Hadija Mpunga Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingim Karume na Mwl. Richard Mkambala shule ya Sekondari George Mkuchika wameipongeza Halmashauri na Wilaya kwa ujumla kwa hatua waliyoichukua ya kuwaongezea hamasa katika ufundishaji pamoja na wanafunzi katika kujifunza kwa kuwa ushindaji wa ufundishaji na ufaulu utaongezeka.

Maadhimisho ya wiki la elimu hufanyika kila mwaka yakiwa na lengo la kutathmini maendeleo ya elimu kwa ngazi ya halmashauri, mkoa na taifa, ambapo Serikali inatoa hamasa kwa wadau kuchangia na kuwekeza katika elimu, kujadili na kuweka mikakati wezeshi ya kuboresha miundombinu kwa maendeleo ya elimu pamoja na kutoa zawadi mbalimbali kwa walimu na wanafunzi waliofanya vizuri.  

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa