• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

ZOEZI LA UTOAJI CHANJO KWA MIFUNGO NG'OMBE 111 MBUZI NA KONDOO 1556 WAMESHAPATIWA CHANJO YA RUZUKU

Posted on: August 26th, 2025

Zoezi la kuchanja mifugo halmashauri ya Mji Newala linaendelea vizuri ambapo mpaka sasa Mbuzi na Kondoo 1556 wamepatiwa chanjo na sotoka pamoja na Ng’ombe 111 wameshapatiwa chanjo ya homa ya mapafu.

Mratibu wa zoezi hilo afisa ugani wa kata ya Nagwala anayeshughulikia mifugo Ndg. Rajabu Killo amesema kuna mwitikio nzuri wa wafugaji ambapo mpaka sasa wameshazifikia kata 8 kati ya 16 kutoa chanjo hiyo ya zuruku.

“Zoezi linaenda vizuri tulianza na Kondoo na Mbuzi kwa kata 8 za hapa mjini mpaka sasa tumechanja mbuzi 1556 na leo tumeanza Ng’ombe tumeshachanja ng’ombe 111 mpaka sasa hatunachangamoto yoyote.” 

Aidha pia Killo amewaomba wananchi wafugaji waendelee kuwaunga mkono kwa kujitokeza kufanikisha utoaji wa chanjo hiyo ili waweze kufikia malengo yaliyowekwa na kuilinda mifugo yao na maradhi yanayoweza kuepukika.

Mmoja wa wafugaji kutoka mtaa wa Nangwala chini Bi. Rose Gadau ameishukuru serikali kwa kuwapunguzia mzigo wa kuhudumia mifugo kwa awali alikua anatumia shilingi 2000 kuchanja ng’ombe mmoja lakini ni shilingi 500 kwa ng’ombe mmoja.

Aidha amewashauri wafugaji wengine kutumia fursa hiyo kwa kuwa zipo hasara mifugo isipopata kinga huku akiiomba serikali kuendelea kuwakumbuka na kuleta chanjo hizo kwa wakati.

“nawaambia wenzangu wafugaji kuchanja sio kwamba tunapata hasara kuna faida, hii chanjo nimeifurahia tunaomba iwe inakuja kwa wakati, kwa sababu mwaka jana mimi nilikuwa na ng’ombe 10 lakini ulipoanza ugonjwa wote walikufa wakabakia hao wawili”.

Idara ya Kilimo, uvuvi na mifugo ya halmashauri ya Mji Newala kwa sasa inaendelea na zoezi la kitaifa la kutoa chanjo na utambuzi mifugo ya Ng’ombe, mbuzi na kondoo.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WADAU WA ELIMU WATAKA USHIRIKIANO ILI KUINUA KIWANGO CHA ELIMU

    August 27, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI CHANJO KWA MIFUNGO NG'OMBE 111 MBUZI NA KONDOO 1556 WAMESHAPATIWA CHANJO YA RUZUKU

    August 26, 2025
  • JESHI LA MAGEREZA NEWALA WACHANGIA DAMU, KUFARIJI WAGONJWA NA KUFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA NEWALA

    August 24, 2025
  • MHE. KUNDYA AWAAGIZA WATAALAM WA KILIMO NA FEDHA KUWAELISHA WAKULIMA KUHUSU UTUNZAJI WA FEDHA

    August 20, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa